Saturday, 15 October 2022

SHULE YA MSINGI MWENGE YAFANYA MAHAFARI YA 80.

 Shule ya Msingi Mwenge yafanya  Sherehe ya kuwaaga wahitimu wa Darasa la saba.Sherehe hii ya kuwaaga Darasa la saba mwaka 2022 ni sherehe ya kihistoria kwani ni sherehe ya 80.

Katika sherehe hii ya kihistoria vipaji mbali mbali vilionyeshwa na wanafunzi wahimu na wanaobaki.

Mgen rasm aliwaasa Wahitimu kuwasaidia wazazi kazi za nyumbani.Pia mgeni Rasmi ameahidi kuwapatia vifaa vya michezo wanafunzi wote walioshiriki michezo kwa ngazi ya mkoa hadi taifa.Mgeni Rasmi Pia ameahid kutengeneza uwanja wa Mpira wa net ball na kutoa zawadi ya mipira kwa shule

Mgeni Rasmi pia ameahidi mifunko 10 ya Sementi kwaajili ya Ujenzi wa Vyoo vya walimu na alitoa hamasa kubwa kwaajili ya kuanza harambee ya ujenzi wa Uzio wa shule hii ili wanafunzi waweze kuwa salama.

Tuesday, 7 June 2022

MAZINGIRA YA SHULE YETU YANAPENDEZA

 Shule yetu ina mazingira safi na yenye kuvutia kwaajili  ya Kujifunza kwa wanafunzi wetu.Tunawakaribisha wote.



Miti ya Vimvuli


Mazingira wezeshi kwa watoto wenye Mahitaji Maalumu


UONGOZI WA SHULE YA MAZOEZI MWENGE

 

MKUU WA SHULE YA MWENGE 
MWL. MASANJA



KAMATI YA SHULE YA MAZOEZI MWENGE

Saturday, 30 October 2021

MATOKEO YA KUHITIMU DARASA LA SABA SHULE YA MWENGE YAZIDI KUFANYA VIZURI ZAIDI.

 Baada ya Matokeo ya darasa la Saba Mwaka 2021 kutangazwa  Shule yetu imezidi kufanya vizuri zaidi kwani imeshika nafasi ya 7 katika Manispaa ya Tabora na Kimkoa imekuwa nafasi ya 12.Kutokana na juhudi kubwa waliyofanya walimu hakuna Mwanafunzi mwenye Wastani wa D na E,Wote wana wastani wa A,B&C.

SOMA ZAID:-    Angalia hapa Matokeo ya Shule ya Mwenge.

Matokeo Darasa la Saba 2021 haya hapa, ufaulu waongezeka

 Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya kuhitimu elimu ya msingi 2021 na kubainisha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 8.89.Akitangaza matokeo hayo leo Jumamosi Oktoba 30, 2021 Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde amesema watahiniwa 907,802 waliofanya mtihani huo wamefaulu.Watahiniwa hawa wamepata alama 121 au zaidi kati ya alama 300” amesema.Amesema kati ya hao wasichana ni 467,967 (asilimia 81.43) na wavulana ni 439,835 (82.56).

Friday, 18 December 2020

Friday, 11 December 2020

SHEREHE MAALUMU YA WALIMU WA SHULE YA MSINGI MWENGE

 Shule ya Msingi Mwenge  tumefanya Sherehe maalumu ya kupongezana kwa matokeo Mazuri ya Darasa la Saba mwaka huu,hii ni baada ya Juhudi kubwa zilizofanywa na walimu wote na kupelekea  kuingia kwenye kumi bora kwa Manispaa ya Tabora.




By Camera Man

E.Jingu


Friday, 13 November 2020

MUONEKANO WA SHULE BAADA YA UKARABATI

 Tunawashukuru wadau wote walioshiriki kwa hali na Mali Kutu_support kwenye ukarabati wetu..